Dar: Dunia imekwisha! Ndiyo sentensi pekee inayoweza kukutoka baada ya kusikia kisa cha binti huyu aliyejitambulisha kwa jina la Malkia Said a.k.a Malkies, mwenye umri wa miaka 19, mkazi wa Magomeni jijini Dar ambaye amekiri kujihusisha na vitendo haramu vya usagaji akieleza alivyotembea na wanawake wenzake wasiopungua 40 wakiwemo wake za watu zaidi ya 20 hadi kufikia hatua ya kufumaniwa na kunyolewa nywele.
Malkies alisema, kwa kuwa anajitambua na anajua nini anachokifanya, alidhani ni vyema kutoka na watu waliomzidi umri kuliko kuwapotosha vijana wa rika lake, ndipo akampata mke wa mtu.
Alisema kabla ya hapo alishakuwa na wake wengine wa watu lakini huyo wa Magomeni hali ilikuwa mbaya kiasi cha kutwangwa talaka na mumewe.
“Nimeshakuwa na wake za watu zaidi ya ishirini, wengi wamenizidi umri pia wake za watu wananitaka wenyewe, huyo mmoja alikuwa anaishi Magomeni na mumewe akawa ananishumbua kwa kipindi kirefu wakati mimi nilikuwa na mtu wangu.
“Nakumbuka ilikuwa mwanzoni mwa mwaka huu, nilipoachana na huyo mtu wangu (mwanamke mwenzake), niliamua kuwa na huyo mwanamke.
“Yeye ana umri wa miaka 30, alinidanganya anaishi na baba yake, akanipeleka hadi kwake. Baadaye aliniweka wazi kuwa anakaa na mumewe na majirani wakamfikishia habari mume wake kuwa huwa nakwenda pale akiwa hayupo.
“Kulitokea ugomvi mkubwa kati ya yule mwanamke na mumewe, yule mwanamke akadai talaka na akapewa kwa sababu yangu.
“Niliendelea naye hata baada ya mumewe kumuacha, tukawa tunaishi wote Ubungo kwa dada yake na mimi nikiwa na mtu najiachia kimahaba siwezi kuficha.
“Wiki mbili baadaye, yule dada’ke alichukia, akaita ndugu zake na yule mume, wakaja kunifumania, wakanipiga na kuninyoa nywele.
“Tuliendelea kidogo lakini sasa tumeachana kabisa,” aliongeza binti huyo ambaye pia aliwahi kushiriki kwenye filamu na muziki japokuwa hakuwika.
STAA ANAYEMZIMIKIA
Akiendelea kueleza kwa kujiamini, Malkies alisema, wanawake wengi ambao alikuwa akiwazimia ni Wazungu na chotara, lakini mbali na hao alikuwa akiumiza kichwa na staa wa filamu za Kibongo, Wema Isaac Sepetu ambaye aliwahi kumtunza Sh. milioni moja kwenye shoo huko Arusha.
“Hakuna msanii anayenivutia zaidi ya Wema na siku ile nilipomtunza ni kwa sababu tu alikuwa amelewa na mimi nililewa, lakini tungekuwa sawa ningemueleza jinsi ninavyomkubali,” alisema.
LENGO LA KUJITANGAZA
Alimalizia kuwa, suala hilo siyo jambo la kufumbia macho kwa sababu linafanywa na wanawake wengi wakiwemo mastaa na wake za watu hivyo ameamua kuanzisha shirika la kuwasaidia wengine ambao bado hawajajiingiza na waliojiingiza kwenye vitendo hivyo ili waache kwa lengo la kuokoa kizazi hiki na kijacho.
Blogger Comment