Shamsa ammwagia sifa JB

Shamsa Ford na JB
MSANII wa Filamu za kibongo, Shamsa Ford, amefunguka kuwa hakuna mtu anayemvutia kwenye tasnia hiyo kama ilivyo kwa msanii mwenzake, Jacob Steven ‘JB’, kutokana na umahiri wake wa kuigiza.
Akizungumza na gazeti hili jana, Shamsa alisema JB ni mtu mmoja ambaye anajua kugusa uhalisia pale anapoigiza na kukitendea haki kipengele hicho.
“JB anaweza kuigiza kama baba wa familia au kijana na akafiti, vilevile akawapendeza mashabiki wake kutokana na kuigiza kwake, napenda kile ambacho anakifanya,” alisema Shamsa.
Alisema hata anapofanya naye kazi huwa wanatengeneza kitu kizuri ambacho mashabiki wao wanakipokea vizuri.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment