GARI la Wema lawekwa Mnadani

WEMA2DAR ES SALAAM: Lile gari la kifahari aina ya Range Rover Evogue lenye namba za usajili AEK 101MP la muigizaji Wema Sepetu ‘Madam’, limewekwa kiporo na madalali wa Yono Auction Mart waliokuwa wakiyapiga bei magari yaliyokamatwa kwa makosa mbalimbali na wenyewe kushindwa kuyakomboa.
Gari hilo lenye thamani ya shilingi milioni 200 lilikamatwa maeneo ya Mbezi-Africana jijini Dar likiwa na msala wa kuingizwa nchini kinyume na utaratibu sambamba na kutolipiwa kodi.
Jumatatu iliyopita, paparazi wetu aliyekuwa na taarifa za mnada huo, aliibuka kwenye yadi ya Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) iliyopo nyuma ya Jengo la Water Front jijini Dar ambapo ilipotimu saa tano na nusu asubuhi, mnada ulianza rasmi.
gari la wema

Kabla ya kuanza mnada huo matajiri zaidi ya hamsini walianza kuyakagua magari yaliyopo kwenye yadi hiyo ingawa mengi yaliyopigwa mnada yalikuwa katika yadi zingine ikiwemo ile ya Baridi, Mnazi Mmoja.
Akizungumza na Risasi Mchanganyiko, mmoja wa wafanyakazi wa Yono Action Mart aliyevalia fulana na kizibao cha kampuni hiyo ambaye alikataa kutaja jina lake, alisema gari hilo zamu yake bado kwani walianza idadi fulani ya magari kutokana na wateja waliojitokeza.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment