Samaki anayezaa kivutio cha watalii Tanzania

 NI samaki wa aina yake anayeishi katika kina kirefu cha maji ya bahari. Ana urefu wa sentimeta 170 na kilogramu 60. Ana mkia wenye ‘mapambo’. Una rangi ya bluu na madoadoa meupe.
Uvumbuzi wake unatajwa kuwa miongoni mwa uvumbuzi wa wanyama wenye kustaajabisha zaidi. Imezoeleka, samaki hutaga mayai kwa ajili ya kuzalisha vifaranga. Lakini kwa samaki huyu, huzaa. Naye si mwingine, bali ni samaki aina ya silikanti. Kwa lugha ya kigeni anajulikana Coelacanth.
Inaelezwa kwamba, mayai ya samaki huyu wa kike hayaanguliwi ndani ya maji. Badala yake, silikanti hutaga mayai mwilini na kuyaangua humohumo au mara tu yanapotoka mwilini huwa ni samaki.
Samaki huyu anapatikana hapa nchini. Huyu ni miongoni mwa vivutio vya utalii vinavyopatikana nchini ndani ya bahari ya Hindi kutoka Tanga hadi Mtwara.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment